Umba sababu njema
UMBA SABABU NJEMA 12 Feb 2026 Mwalimu: Amani Ernest Kyamba SOGH team Let's do GOD'S work together. YESU alipokuwa anasulubiwa pale msalabani, shetani pamoja na wanadamu waliona wanamuua YESU. Kwamba ndo mwisho wa mwokozi, wakati huo YESU alikuwa anaumba sababu njema kuwa analitimiza andiko, na pia anamaliza kazi iliyomleta kwani alizaliwa ili afe kwa kusulubiwa kwa ajili yetu. Shetani aliyajua maandiko, ko labda naye angekuwa kipaumbele kuzuia YESU asisulubiwe lakini shetani ndo akasapoti kwani na yeye shetani yupo kwenye uwepo wa MUNGU, anafanya kazi ya MUNGU japo hapati thawabu kwa sababu ya makosa aliyoyafanya. Hata na sisi tukiwa tunafanya matendo ya uzima, kwa kujifariji kama sauli alivyojifariji kuwa heri ng'ombe na vinono visife kuliko kufa, Eti Bwana ana njaa ya sadaka. Sauli alihisi kuwa MUNGU ni masikini na anahitaji vitu vyake, kumbe MUNGU anahitaji utii wake. Tukiwa kama "sauli na shetani" basi tutafanya mambo yapasayo thawabu ila hatutapata th...