Posts

Showing posts from February, 2026

Part 02:KIVULI CHA YAJAYO

 Kabla haujasoma ujumbe huu,itapendeza ukisoma sehemu ya kwanza ya hili somo linaitwa KIVULI CHA YAJAYO. Unaweza kulisoma kabla ya hii part 02 ili tuweze kupata ujumbe uliokamilika zaidi. Kwanza nimalizie somo lililopita kwa kitu kimoja.   Ufalme wa MUNGU(wokovu) utashuka kwetu pale tu kwanza tukikubali udhaifu na kuhitaji msaada.udhaifu ni Sheria ya torati.ko kamwe hatutastahili agano la wokovu kama hatujakubali kufuata Sheria ya MUNGU kwanza na kushindwa...(Tunajifunza zaidi) Luka 17:20-21 Tunaona kuwa ufalme wa MUNGU ulikuwa katika Israel kwanza kutokana na uwepo wa torati(Sheria). ufalme inamaanisha utawala ko inamaanisha kwamba ukianza kujitahidi kuzifuata Sheria za MUNGU Kuna dalili kwamba unatawaliwa na MUNGU.ko inamaanisha kwamba lazima tuzifuate Sheria za MUNGU kwanza hapo ndipo ufalme(utawala) wa MUNGU utakuwa kwetu. Mathayo 21:43 lakini YESU anakuja kusema Tena kwamba ufalme wa MUNGU utaondolewa kwenu kwa kuwa hamzai matunda ya kifalme na watapewa watu wengine..hii ...

Part 01:KIVULI CHA YAJAYO

 My name:Amani Ernest Kyamba  SOGH Team  Let's do GOD'S work together  Kwenye Lile somo lililopita la "KWA NINI UMEOKOKA" tulizungumzia watu waliopambana na ya chini wakashindwa basi nilibakisha mfano mmoja wa mtu aliyeshindana na Nuru akaishinda yakobo alipambana na MUNGU wa mbinguni aliposhinda akapata baraka kubwa kuliko wote duniani.mshinde MUNGU uteke ufalme wake maana ufalme wa MUNGU unapatikana kwa nguvu na kuuteka. Na siyo kuwa na lengo la kushindana na ulimwengu.maana YESU alishinda ulimwengu sio kwa kushindana nao Bali kwa kutoa mfano wa kujitoa kikamilifu mbele za MUNGU.ndipo akaishinda. part 01: PALIPO NA UDHAIFU PANA NGUVU Lengo la haya masomo ni kuwafumbua  wakristo waanze kuona mambo ya rohoni kujua walipotoka walipo na wanapokwenda..maana watu wengine wanasema wametoka mbali huku kumbe walipo ndo waliipotoka hapo walipo ukiwa hivyo basi maana yake mtu unakuwa kipofu yaani usiyeona chochote.YESU.kristo anataka tuone, kwamba macho yafumbuke tujue t...

Umba sababu njema

UMBA SABABU NJEMA     Mwalimu: Amani Ernest Kyamba   SOGH team  Let's do GOD'S work together.   YESU alipokuwa anasulubiwa pale msalabani, shetani pamoja na wanadamu waliona wanamuua YESU. Kwamba ndo mwisho wa mwokozi, wakati huo YESU alikuwa anaumba sababu njema kuwa analitimiza andiko, na pia anamaliza kazi iliyomleta kwani alizaliwa ili afe kwa kusulubiwa kwa ajili yetu. Shetani aliyajua maandiko, ko labda naye angekuwa kipaumbele kuzuia YESU asisulubiwe lakini shetani ndo akasapoti kwani na yeye shetani yupo kwenye uwepo wa MUNGU, anafanya kazi ya MUNGU japo hapati thawabu kwa sababu ya makosa aliyoyafanya.          Hata na sisi tukiwa tunafanya matendo ya uzima, kwa kujifariji kama sauli alivyojifariji kuwa heri ng'ombe na vinono visife kuliko kufa, Eti Bwana ana njaa ya sadaka. Sauli alihisi kuwa MUNGU ni masikini na anahitaji vitu vyake, kumbe MUNGU anahitaji utii wake.     Tukiwa kama "sauli na shetani...

Je kwa nini namna ile?

Swali: hakukuwa na njia nyingine mbadala ya kutuokoa sisi mpaka YESU afe? ​ Amani Ernest Kyamba  SOGH Team . ​Let's do GOD'S work together . ​Njia zilikuwepo nyingi kwa sababu MUNGU ni mtendaji na muweza wa yote. Kwa hiyo MUNGU alitaka atumie njia ile ile ya wokozi sawasawa na njia ya uharibifu. Yaani alitaka/alipanga kumrudisha mwanadamu katika utakatifu sawasawa na njia ambayo mwanadamu aliingia katika upotevu. ​Adamu na Eva walipotea kwa kutokutii. YESU akaonyesha njia ya utii katika maisha yaliyozungukwa na kukosa utiifu, Luka 2:52, (akamtii MUNGU na wanadamu) Pamoja na kwamba mwanadamu hakutii na alizama dhambini yeye YESU akampa chaguo mwanadamu, la kukosa utii au kuamua kutii/kufanywa mtiifu. Kwani kupitia yeye mwanadamu akatambulishwa kwamba inawezekana kuwa mtii.  ​Kutokutii kwa Adamu kulisababisha kifo. Kifo cha YESU kilimpa mwanadamu nafasi ya kumtii na kumtumikia MUNGU.  Adamu alikula tunda akafa, YESU alikufa akaishi.  Adamu alifukuzwa kwenye urit...

nani unayemuangalia?

Tunajenga nia kwa ajili ya nani?   SOGH Team Amani Ernest Kyamba.  Let's do GOD'S work together.   Note: Hili somo nimetumia reference ya cgm (christ gospel messenger) iliyopo kanisa la EAGT. Mimi nasali EAGT saza songwe kwa Daudi Before mbeyeye (true pastor). Hii haionyeshi mapungufu ya kanisani kwetu, ila nikaona nijifunze zaidi kupitia hali ambayo nadhani wengi wanaipitia kiroho na kimwili. #sisi tupo vizuri zaidi na tunapambana ili tuione mbingu pamoja na viongozi wetu wa kiroho (mchungaji na wazee wetu wa kanisa). Nimeona ni vyema nitumie mfano wa mazingira yangu ili hatimaye wote tuwe vizuri kabisa.         Mara nyingi tunafanya mambo ya rohoni kwa kutumia reference fulani, yaani tuna copy. Jambo ambalo siyo. Tusiwape wanadamu wenzetu hali ya kwamba tunakopi kila kitu toka kwao kwa kuwa yale yalikuwa ni wakati ule (kwa mwanadamu) japo MUNGU ni yule yule.      kwa mfano nilisikia mfano kutoka kwa kaka kwamba CGM ya za...

Ole

​05 Feb 2025 Ole kwetu sisi watumishi wa MUNGU ​nilikutana na watu wabaya wenye utisho porini na yote ni kwa kuwa kwanza nilipanda gari binafsi (nilijitenga na wenzangu waliokuwa kwenye basi mithali 18:1) na wakati huo nilikuwa na begi la thamani mno ambalo ni neno la MUNGU. ​Njiani porini nikashangaa begi limedondoka lenyewe kwanza kwa kuwa halikunistahili Mimi kushuka tu kumbe wale wa gari binafsi walikuwa dili moja na wale watu wa porini wanaotisha ambao walibeba visu, na vifaa vikali ili wanitishe.   ​Begi Lile sikuliona Wala chochote sikuliona nilipoteza neno ila ujuzi wa kupika sikupoteza basi shetani anahitaji ujuzi wangu wa kupika ko akaniambia nikapike chakula (junk) kinachoangamiza na kinachovutia. mimi nikajitambulisha kuwa Mimi ni mtumishi wa MUNGU wakasema kuwa hata wao Wana MUNGU wao, Mimi nikasema ni MUNGU wa mbinguni wakasema hata wao ni hivyohivyo..   ​Kumbe shetani anaweza akajigeuza kuwa malaika wa nuru ili kukupata wewe ambaye unajua neno la MUNGU...

Msingi imara(short notes)

​1. Kanisa na Msingi Imara ​ 07 Jun 2024 Kanisa na msingi imara. ​Hakuna nyumba inayojengwa pasipo msingi. uimara wa msingi ndio unaoamua uwezo wa nyumba kuhimili mabadiliko ya Hali ya hewa. ina maana kama kanisa linachezewa na shetani Ina maana kuwa kanisa halina msingi imara. makanisa mengi ya Sasa hayana msingi imara wa wokovu, yaani watu Wana sali lakini Wana hila mioyoni mwao, yaani kwaya zina ugomvi, na watu Wana maneno na hila wao kwa wao, watu wengini ni wasengenyaji uwepo wa dhambi katika kanisa unamuondoa MUNGU asiwepo kwenye kanisa Hilo na ndio maana ibada inapoa na watu wanabaki vile vile siku zote kwa Sababu mtu asiye na MUNGU anafananishwana jiwe ndani ya maji linalokaa kwenye maji ila haliruhusu maji kuingia ndani, yaani mwenye dhambi hawezi kumwona MUNGU hata siku Moja mpaka MUNGU atakapogeuza moyo wa mtu huyo uwe wa nyama. uwepo wa dhambi na kukosa utii wa neno la MUNGU kwa watu unaondoa uwepo wa MUNGU kwenye kanisa. ​ #yoshua 7:1. israeli ni mfano wa kanisa kam...

Mwamuzi(short notes)

​3. Nani amekufanya mwamuzi kwetu? ​ 20 Jan 2025 Nani amekufanya mwamuzi kwetu?//ijue thamani ya mwamuzi. Kutoka 2:14. ​Kwa Nini mwamuzi akati wamezoea utumwa.mwamuzi alikuja kwa lengo la kuonyesha Nia ya kuwasaidia lakini wao wanamshangaa na kumwona kama anajipendekeza. #MUNGU wa mbinguni amewavusha Israel kwenda nchi ya ahadi, lakini Wana wa Israel wanamshangaa Musa na MUNGU kwamba kwa Nini wamewatoa misri, kwa kuwa shida ya misri waliiona kuwa ni Raha. #na sisi utumwa wa dhambi tunauona ni Uhuru na uzuri kwetu. ​Mfano mwingine: 1 samweli 23:1-13. Daudi aliwaokoa keila kutoka katika mikono ya wafilisti, lakini keila walikuwa wanaenda kumsaliti Daudi kwa kuwa hawakutambua thamani ya mwamuzi. ​YESU Kristo ni mwamuzi!! Unaijua thamani yake?  Kuudharau wokovu ni dalili tosha kuwa. Harutambui thamani ya mwamuzi(YESU kristo) Tutapataje kupona tusipoujali wokovu mkuu namna hii. Wao waliijua thamani,kwa nini sisi tusiijue? Tunapaswa kuijua,ili tusije tukakataliwa japo tuliku...

Kuitambua neema(short notes)

​ 24 Sep 2024 Jinsi ya kuulinda utakatifu ​Utakatifu ni usafi kuanzia ndani (mawazo) mpaka nje. yaani mbegu ya mhindi haiwezi kuotesha maharage hivyo kama una mawazo ya kufisha ndani ya akili haijalishi unajizuiaje Bado hujashinda kwa kuwa utakatifu wa kweli unaanzia ndani. ​Unajua kwa Nini Wana wa Israel walishindwa kulifuata Sheria ni kwakuwa walitaka kuwa wazuri lakini chemichemi za mioyo yao zilitoa mambo maovu,, ikijaa chemichemi lazima maovu yatadhihirika na ndio maana tukiishi katika wokovu wa Sheria tunatoa maovu yaani tunaondoa maji ya chemichemi chafu ko yanaanza kujaaa Tena.. mda wote huo tutajiona watakatifu na wenye kumpendeza MUNGU lakini pale tu chemichemi ikijaa uovu unadhihirisha nguvu tukaanguka tena. ​ Warumi 7:15.. ​Je Nini tufanye ili tukamilike katika utakatifu? Ni kwa kufisha chemichemi chafu za asili ya Dunia hii za dhambi kwa kujitoa kikamilifu kwa MUNGU kupitia YESU Warumi 12:1.. kwa kuvuviwa (kuunda kiu ya kuacha dhambi) ambako ndiko kunamwita RO...

Ukuta wa moto

​14 Sep 2024 Kibali Cha kukua/je UKUTA wa moto unakufaaa? ​Ni sawa na simulizi Moja inahusu mtu mwenye silaha za kushinda ila hajajipanga kushinda...yaani katika vita na utumwa uliokuwapo kwa maeneo kutumikishwa na wavamizi yeye alikuwa na silaha Kali sana ambazo yakini zingeweza kuwapa hao wenzake uhuru lakini yeye akaona Bora utumwa kuliko kujitoa kwa ajili ya wengine.   ​*Tunakuja kuona jinsi watu wamevaa silaha zote ila sio utayari,, utayari tunauunda sisi na MUNGU akiuona anatufungia kwa miguu,, anatuvisha Sasa ili miguu yetu ipate kibali Cha kuanza vita.   ​*apandaye Wala amwagiliaye maji SI kitu Bali akuzaye. 1 korinto 3:7 tumapandwa na watumishi wa MUNGU katika shamba la MUNGU kupitia neno la injili..maji tunamwagiliwa kwa mafundisho ya ualimu na maisha ndani ya wokovu...   ​Ni sawa ila je Nini kitakacho mkuza mtu 1 korinto 3:8 baada ya kukamilika kwa matunzo ya mmea basi suala la roho ya mtu kukua linabaki kuwa la mtu mwenyewe na MUNGU wa mbinguni....

Kumpenda MUNGU kwa yote

Hii ni mwendelezo wa somo la "usijidharau" ​ 12 Jan 2025 Kumpenda BWANA YESU kwa vyote. (Part 02 ya usijidharau) ​ Mathayo 22:37. ​Yule mtu YESU akampenda kwa kuwa amezishika amri zake na kwa kweli alikuwa anamtumikia MUNGU. ​.    yesu akampenda sana mno akatabasamu akafurahi na pia akamwonea huruma. ​.      akaona upendo wake kwa kweli umewekeza kwenye vyote kasoro Mali zake kwa upendo wake YESU akataka amkamilishe hicho kimoja akamwambia gawa nusu ya Mali zako uwagawie maskini hapo utakuwa kamili yule mtu akaondoka kwa huzuni nyingi kwani alijijuwa kuwa kweli hajakamilika!!.         hata pale YESU alikuwa anaangalia wanavyotoa sadaka akawa anaupima upendo na sio utajiri ndo uliowafanya wale matajiri wasimwone MUNGU kwa kuwa kutoa kwao kulikuwa ni kwa Sababu ya utukufu wao kwa watu na sio upendo na moyo wa kimungu, ila yule mama mjane alitoa sadaka ya moyo. maana moyo wako ulipo ndipo na sadaka Yako itakapokuwapo mathayo 6:19-2...

Uvuvio

​22 Jan 2025 Uvuvio Fellow SOGH: Amani Ernest Kyamba.   ​Maombi sahihi ni kuomba uvuvio. uvuvio ni kama vile kuchukua kibali kwa yanayoenda kufanyika.   ​#YESU aliwavuvia (alitamka) ROHO mtakatifu wanafunzi wake (Hadi sisi). yaani alipotamka ni kwamba aliweka muhuri kwamba tukikidhi maandalio ya moyo kumpokea ROHO MTAKATIFU ni haki yetu kuongozwa naye ROHO MTAKATIFU.   ​Fellow SOGH: Amani Ernest Kyamba.   ​#ko hata uamsho hatitaomba uamsho lakini kabla ya matendo ya uamsho tunavuvia kupitia jina la YESU Kristo kwamba yanayoenda kutendeka yapate kibali mbele za hayo matendo ya uamsho.   ​#sulemani alivuvia hekalu alilojenga kwa ajili ya BWANA. Na uvuvio wa sulemani ukatimizwa kwani ndo ikawa hivyo 1 falme 8:22-61. pale ni kwamba sulemani alikuwa anavuvia hekalu la BWANA.   ​Uvuvio unaleta uhalali. ko hata sisi tunanung'unika kwamba huduma zetu hazikui ni kwakuwa hatujavuvia ukuaji. kwamba tunapoanza vitendo vya kukuza huduma (ku...

Yule pepo akamtia kifafa

​15 Sep 2024 ​Yule Pepo akamtia kifafa akamtoka ​Luka 9:41 Marko 1:25 Marko 9:25 ​Lengo la Pepo kumtia kifafa yule mtu ni kupima uponyaji wa yule mtu kwamba mtu ajione mtumwa akati yupo huru.   ​     pepo alitoka Pepo ni kama nguruwe. tukifuga uovu ni mfano wa kufuga nguruwe. nguruwe ni mchafu sana, na ndiye anayezalisha uchafu kwenye zizi lake. kazi ya YESU unapoomba ni kuondoa chanzo Cha uchafu ambao ndio Pepo, lakini ukiondoa nguruwe Bado zizi litabaki chafu ko itaonesha kwamba hapa palikuwako na nguruwe.   ​      kuondoa huo uchafu ni kuanza mahusiano na MUNGU uchafu Baki wote utaondoka.         wengine wanaondoa uchafu huku nguruwe Bado IPO, hapo itakuwa ni kuteseka, maana Bado chanzo kipo kinatusumbua.   ​#watu wameokoka na wanateseka na matendo ya Giza, lakini hawana Pepo na wanajishuhudia kabisa kuwa hawana pepo, lakini wanateseka na tamaa na dhambi, ni kwa Sababu uchafu uliobaki hausafishwi, Bado wa...