Posts

Showing posts from February, 2026

Umba sababu njema

UMBA SABABU NJEMA 12 Feb 2026 Mwalimu: Amani Ernest Kyamba SOGH team Let's do GOD'S work together. YESU alipokuwa anasulubiwa pale msalabani, shetani pamoja na wanadamu waliona wanamuua YESU. Kwamba ndo mwisho wa mwokozi, wakati huo YESU alikuwa anaumba sababu njema kuwa analitimiza andiko, na pia anamaliza kazi iliyomleta kwani alizaliwa ili afe kwa kusulubiwa kwa ajili yetu. Shetani aliyajua maandiko, ko labda naye angekuwa kipaumbele kuzuia YESU asisulubiwe lakini shetani ndo akasapoti kwani na yeye shetani yupo kwenye uwepo wa MUNGU, anafanya kazi ya MUNGU japo hapati thawabu kwa sababu ya makosa aliyoyafanya. Hata na sisi tukiwa tunafanya matendo ya uzima, kwa kujifariji kama sauli alivyojifariji kuwa heri ng'ombe na vinono visife kuliko kufa, Eti Bwana ana njaa ya sadaka. Sauli alihisi kuwa MUNGU ni masikini na anahitaji vitu vyake, kumbe MUNGU anahitaji utii wake. Tukiwa kama "sauli na shetani" basi tutafanya mambo yapasayo thawabu ila hatutapata th...

Je kwa nini namna ile?

M ​ ​Swali: hakukuwa na njia nyingine mbadala ya kutuokoa sisi mpaka YESU afe? ​Amani Ernest Kyamba SOGH Team. ​Let's do GOD'S work together. ​Njia zilikuwepo nyingi kwa sababu MUNGU ni mtendaji na muweza wa yote. Kwa hiyo MUNGU alitaka atumie njia ile ile ya wokozi sawasawa na njia ya uharibifu. Yaani alitaka/alipanga kumrudisha mwanadamu katika utakatifu sawasawa na njia ambayo mwanadamu aliingia katika upotevu. ​Adamu na Eva walipotea kwa kutokutii. YESU akaonyesha njia ya utii katika maisha yaliyozungukwa na kukosa utiifu, Luka 2:52, (akamtii MUNGU na wanadamu). Pamoja na kwamba mwanadamu hakutii na alizama dhambini yeye YESU akampa chaguo mwanadamu, la kukosa utii au kuamua kutii/kufanywa mtiifu. Kwani kupitia yeye mwanadamu akatambulishwa kwamba inawezekana kuwa mtii. ​Kutokutii kwa Adamu kulisababisha kifo. Kifo cha YESU kilimpa mwanadamu nafasi ya kumtii na kumtumikia MUNGU. Adamu alikula tunda akafa, YESU alikufa akaishi. Adamu alifukuzwa kwenye urithi wake, Y...

SOGH Team: nani unayemuangalia?

Tunajenga nia kwa ajili ya nani? SOGH Team Amani Ernest Kyamba. Let's do GOD'S work together. Note: Hili somo nimetumia reference ya cgm (christ gospel messenger) iliyopo kanisa la EAGT. Mimi nasali EAGT saza songwe kwa Daudi Before mbeyeye (true pastor). Hii haionyeshi mapungufu ya kanisani kwetu, ila nikaona nijifunze zaidi kupitia hali ambayo nadhani wengi wanaipitia kiroho na kimwili. #sisi tupo vizuri zaidi na tunapambana ili tuione mbingu pamoja na viongozi wetu wa kiroho (mchungaji na wazee wetu wa kanisa). Nimeona ni vyema nitumie mfano wa mazingira yangu ili hatimaye wote tuwe vizuri kabisa. Mara nyingi tunafanya mambo ya rohoni kwa kutumia reference fulani, yaani tuna copy. Jambo ambalo siyo. Tusiwape wanadamu wenzetu hali ya kwamba tunakopi kila kitu toka kwao kwa kuwa yale yalikuwa ni wakati ule (kwa mwanadamu) japo MUNGU ni yule yule. #kwa mfano nilisikia mfano kutoka kwa kaka kwamba CGM ya zamani ilikuwa moto tofauti na sasa. Ni sawa na ni kweli lak...

Ole

​05 Feb 2025 Ole kwetu sisi watumishi wa MUNGU ​nilikutana na watu wabaya wenye utisho porini na yote ni kwa kuwa kwanza nilipanda gari binafsi (nilijitenga na wenzangu waliokuwa kwenye basi mithali 18:1) na wakati huo nilikuwa na begi la thamani mno ambalo ni neno la MUNGU. ​Njiani porini nikashangaa begi limedondoka lenyewe kwanza kwa kuwa halikunistahili Mimi kushuka tu kumbe wale wa gari binafsi walikuwa dili moja na wale watu wa porini wanaotisha ambao walibeba visu, na vifaa vikali ili wanitishe.   ​Begi Lile sikuliona Wala chochote sikuliona nilipoteza neno ila ujuzi wa kupika sikupoteza basi shetani anahitaji ujuzi wangu wa kupika ko akaniambia nikapike chakula (junk) kinachoangamiza na kinachovutia. mimi nikajitambulisha kuwa Mimi ni mtumishi wa MUNGU wakasema kuwa hata wao Wana MUNGU wao, Mimi nikasema ni MUNGU wa mbinguni wakasema hata wao ni hivyohivyo..   ​Kumbe shetani anaweza akajigeuza kuwa malaika wa nuru ili kukupata wewe ambaye unajua neno la MUNGU...

Msingi imara(short notes)

​1. Kanisa na Msingi Imara ​ 07 Jun 2024 Kanisa na msingi imara. ​Hakuna nyumba inayojengwa pasipo msingi. uimara wa msingi ndio unaoamua uwezo wa nyumba kuhimili mabadiliko ya Hali ya hewa. ina maana kama kanisa linachezewa na shetani Ina maana kuwa kanisa halina msingi imara. makanisa mengi ya Sasa hayana msingi imara wa wokovu, yaani watu Wana sali lakini Wana hila mioyoni mwao, yaani kwaya zina ugomvi, na watu Wana maneno na hila wao kwa wao, watu wengini ni wasengenyaji uwepo wa dhambi katika kanisa unamuondoa MUNGU asiwepo kwenye kanisa Hilo na ndio maana ibada inapoa na watu wanabaki vile vile siku zote kwa Sababu mtu asiye na MUNGU anafananishwana jiwe ndani ya maji linalokaa kwenye maji ila haliruhusu maji kuingia ndani, yaani mwenye dhambi hawezi kumwona MUNGU hata siku Moja mpaka MUNGU atakapogeuza moyo wa mtu huyo uwe wa nyama. uwepo wa dhambi na kukosa utii wa neno la MUNGU kwa watu unaondoa uwepo wa MUNGU kwenye kanisa. ​ #yoshua 7:1. israeli ni mfano wa kanisa kam...

Mwamuzi(short notes)

​3. Nani amekufanya mwamuzi kwetu? ​ 20 Jan 2025 Nani amekufanya mwamuzi kwetu?//ijue thamani ya mwamuzi. Kutoka 2:14. ​Kwa Nini mwamuzi akati wamezoea utumwa.mwamuzi alikuja kwa lengo la kuonyesha Nia ya kuwasaidia lakini wao wanamshangaa na kumwona kama anajipendekeza. #MUNGU wa mbinguni amewavusha Israel kwenda nchi ya ahadi, lakini Wana wa Israel wanamshangaa Musa na MUNGU kwamba kwa Nini wamewatoa misri, kwa kuwa shida ya misri waliiona kuwa ni Raha. #na sisi utumwa wa dhambi tunauona ni Uhuru na uzuri kwetu. ​Mfano mwingine: 1 samweli 23:1-13. Daudi aliwaokoa keila kutoka katika mikono ya wafilisti, lakini keila walikuwa wanaenda kumsaliti Daudi kwa kuwa hawakutambua thamani ya mwamuzi. ​YESU Kristo ni mwamuzi!! Unaijua thamani yake?  Kuudharau wokovu ni dalili tosha kuwa. Harutambui thamani ya mwamuzi(YESU kristo) Tutapataje kupona tusipoujali wokovu mkuu namna hii. Wao waliijua thamani,kwa nini sisi tusiijue? Tunapaswa kuijua,ili tusije tukakataliwa japo tuliku...

Kuitambua neema(short notes)

​ 24 Sep 2024 Jinsi ya kuulinda utakatifu ​Utakatifu ni usafi kuanzia ndani (mawazo) mpaka nje. yaani mbegu ya mhindi haiwezi kuotesha maharage hivyo kama una mawazo ya kufisha ndani ya akili haijalishi unajizuiaje Bado hujashinda kwa kuwa utakatifu wa kweli unaanzia ndani. ​Unajua kwa Nini Wana wa Israel walishindwa kulifuata Sheria ni kwakuwa walitaka kuwa wazuri lakini chemichemi za mioyo yao zilitoa mambo maovu,, ikijaa chemichemi lazima maovu yatadhihirika na ndio maana tukiishi katika wokovu wa Sheria tunatoa maovu yaani tunaondoa maji ya chemichemi chafu ko yanaanza kujaaa Tena.. mda wote huo tutajiona watakatifu na wenye kumpendeza MUNGU lakini pale tu chemichemi ikijaa uovu unadhihirisha nguvu tukaanguka tena. ​ Warumi 7:15.. ​Je Nini tufanye ili tukamilike katika utakatifu? Ni kwa kufisha chemichemi chafu za asili ya Dunia hii za dhambi kwa kujitoa kikamilifu kwa MUNGU kupitia YESU Warumi 12:1.. kwa kuvuviwa (kuunda kiu ya kuacha dhambi) ambako ndiko kunamwita RO...

Madhabahu.(short notes)

​ 10 Aug 2024 Kwa Nini ni muhimu kuhudhuria kanisani/kanisa ni madhabahu, madhabahu sahihi ya MUNGU. ​Kwanza kabisa lazima tujue kuwa ni Nini maana ya madhabahu? Kabla ya yote ngoja tuone madhabahu ya kwanza katika biblia ikijengwa kwa ajili ya nini? Yaani tutambue umuhimu wa madhabahu. ​Ko kumbe madhabahu ndiyo itakayotuunganisha na MUNGU. ​*Madhabahu ya kwanza kabisa katika biblia ilijengwa na nuhu. Katika mwanzo 8:20-23. ukiachana na lle madhabahu ya kwanza ya akina kaini na habili. ​*Nguvu ya madhabahu ilimfanya MUNGU aamue kubadilisha Nia ya kuja kuipiga Dunia kwa mapigo makuu kwa Sababu ya dhambi, yaani baada ya nuhu kutoa sadaka ya kuteketezwa kwa MUNGU kupitia viumbe hai safı vilivyokuwepo ndani ya safina ndipo mahali ambapo BWANA MUNGU aliviongezea thamani viumbe vyote katika Dunia kwa kuanza na mwanadamu wake. ko msamaha wa kwanza wa Dunia wa siku zote ulianza kwa Sababu ya madhabahu. ​*Ko kumbe tunakuja kujua kwamba madhabahu ni sehemu ya upatanisho kati ya MUNGU ...

Ukuta wa moto

​14 Sep 2024 Kibali Cha kukua/je UKUTA wa moto unakufaaa? ​Ni sawa na simulizi Moja inahusu mtu mwenye silaha za kushinda ila hajajipanga kushinda...yaani katika vita na utumwa uliokuwapo kwa maeneo kutumikishwa na wavamizi yeye alikuwa na silaha Kali sana ambazo yakini zingeweza kuwapa hao wenzake uhuru lakini yeye akaona Bora utumwa kuliko kujitoa kwa ajili ya wengine.   ​*Tunakuja kuona jinsi watu wamevaa silaha zote ila sio utayari,, utayari tunauunda sisi na MUNGU akiuona anatufungia kwa miguu,, anatuvisha Sasa ili miguu yetu ipate kibali Cha kuanza vita.   ​*apandaye Wala amwagiliaye maji SI kitu Bali akuzaye. 1 korinto 3:7 tumapandwa na watumishi wa MUNGU katika shamba la MUNGU kupitia neno la injili..maji tunamwagiliwa kwa mafundisho ya ualimu na maisha ndani ya wokovu...   ​Ni sawa ila je Nini kitakacho mkuza mtu 1 korinto 3:8 baada ya kukamilika kwa matunzo ya mmea basi suala la roho ya mtu kukua linabaki kuwa la mtu mwenyewe na MUNGU wa mbinguni....

Kumpenda MUNGU kwa yote

Hii ni mwendelezo wa somo la "usijidharau" ​ 12 Jan 2025 Kumpenda BWANA YESU kwa vyote. (Part 02 ya usijidharau) ​ Mathayo 22:37. ​Yule mtu YESU akampenda kwa kuwa amezishika amri zake na kwa kweli alikuwa anamtumikia MUNGU. ​#yesu akampenda sana mno akatabasamu akafurahi na pia akamwonea huruma. ​#akaona upendo wake kwa kweli umewekeza kwenye vyote kasoro Mali zake kwa upendo wake YESU akataka amkamilishe hicho kimoja akamwambia gawa nusu ya Mali zako uwagawie maskini hapo utakuwa kamili yule mtu akaondoka kwa huzuni nyingi kwani alijijuwa kuwa kweli hajakamilika!!. ​#hata pale YESU alikuwa anaangalia wanavyotoa sadaka akawa anaupima upendo na sio utajiri ndo uliowafanya wale matajiri wasimwone MUNGU kwa kuwa kutoa kwao kulikuwa ni kwa Sababu ya utukufu wao kwa watu na sio upendo na moyo wa kimungu, ila yule mama mjane alitoa sadaka ya moyo. maana moyo wako ulipo ndipo na sadaka Yako itakapokuwapo mathayo 6:19-21. mama moyo wake ulikuwapo kwa MUNGU ko na sadaka...

Uvuvio

​22 Jan 2025 Uvuvio Fellow SOGH: Amani Ernest Kyamba.   ​Maombi sahihi ni kuomba uvuvio. uvuvio ni kama vile kuchukua kibali kwa yanayoenda kufanyika.   ​#YESU aliwavuvia (alitamka) ROHO mtakatifu wanafunzi wake (Hadi sisi). yaani alipotamka ni kwamba aliweka muhuri kwamba tukikidhi maandalio ya moyo kumpokea ROHO MTAKATIFU ni haki yetu kuongozwa naye ROHO MTAKATIFU.   ​Fellow SOGH: Amani Ernest Kyamba.   ​#ko hata uamsho hatitaomba uamsho lakini kabla ya matendo ya uamsho tunavuvia kupitia jina la YESU Kristo kwamba yanayoenda kutendeka yapate kibali mbele za hayo matendo ya uamsho.   ​#sulemani alivuvia hekalu alilojenga kwa ajili ya BWANA. Na uvuvio wa sulemani ukatimizwa kwani ndo ikawa hivyo 1 falme 8:22-61. pale ni kwamba sulemani alikuwa anavuvia hekalu la BWANA.   ​Uvuvio unaleta uhalali. ko hata sisi tunanung'unika kwamba huduma zetu hazikui ni kwakuwa hatujavuvia ukuaji. kwamba tunapoanza vitendo vya kukuza huduma (ku...

Yule pepo akamtia kifafa

​15 Sep 2024 ​Yule Pepo akamtia kifafa akamtoka ​Luka 9:41 Marko 1:25 Marko 9:25 ​Lengo la Pepo kumtia kifafa yule mtu ni kupima uponyaji wa yule mtu kwamba mtu ajione mtumwa akati yupo huru.   ​#pepo alitoka Pepo ni kama nguruwe. tukifuga uovu ni mfano wa kufuga nguruwe. nguruwe ni mchafu sana, na ndiye anayezalisha uchafu kwenye zizi lake. kazi ya YESU unapoomba ni kuondoa chanzo Cha uchafu ambao ndio Pepo, lakini ukiondoa nguruwe Bado zizi litabaki chafu ko itaonesha kwamba hapa palikuwako na nguruwe.   ​#kuondoa huo uchafu ni kuanza mahusiano na MUNGU uchafu Baki wote utaondoka. #wengine wanaondoa uchafu huku nguruwe Bado IPO, hapo itakuwa ni kuteseka, maana Bado chanzo kipo kinatusumbua.   ​Fellow SOGH Amani Ernest Kyamba. ​#watu wameokoka na wanateseka na matendo ya Giza, lakini hawana Pepo na wanajishihudia kabisa kuwa hawana pepo, lakini wanateseka na tamaa na dhambi, ni kwa Sababu uchafu uliobaki hausafishwi, Bado wanaendelea kuufuga ndani ko Bado ...

Usijidharau

​ 31 Aug 2024 Hili ni part 02 ya somo linaloitwa "usijiamini". ​ Usijidharau kwa Hali Yako ya sasa, sisi wote ni sawa./wito wa MUNGU. ​ This is a SOGH Amani Ernest Kyamba ​Gharama tuliyonayo kuyapata maisha ndo hiyo hiyo ambayo tajiri anayo kuyapoteza maisha yake. Luka 18:20-23 yule tajiri aliifuata Sheria alijitoa kwelikweli lakini Kuna mahali pamoja tu hakujitoa (Mali yake halikuwa imeokoka). YESU akamwambia kwamba ili ukidhi viwango vya kumfwata YESU ni lazima kwanza uuze ulivyonavyo yule mtu akahuzunika kwa kuwa alikuwa na Mali nyingi (endapo zingekuwa chache angetoa kwa urahisi kabisa lakini wingi wa Mali ndio ukaongeza wingi wa ugumu wa kumfuata YESU. ​#na YESU akasema ni rahisi ngamia kupitia kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa MUNGU. ​*Mjane sadaka yake ilikubaliwa kwa Sababu ya ukamilifu wa moyo wake kwa MUNGU. kwa kuwa sadaka ya kwanza inayohalalisha sadaka zingine zote ni utakatifu. ​*Wale matajiri walitoa vingi vyenye maana la...

Jumbe kwa makanisa saba

​16 Jun 2024   ​Jumbe Saba kwa makanisa ya leo   ​By amani Ernest Kyamba. From SOGH team.   ​.hapa Cha kwanza tunabidi tujue kuwa kanisa ni hekalu la MUNGU ambalo ndilo sisi. 1 korinto 3:16   ​*Kumbe huu ujumbe wa makanisa saba haya ni ujumbe wa mtu mmoja mmoja kwanza ndipo itafuata sinagogi maana sinagogi lisilo na mapungufu linajengwa na watu wasio na mapungufu pia. ko kumbe utimilifu wa sinagogi unaanza na sisi wenyewe.   ​Kitabu Cha ufunuo kilikuwa kinalifumbua kanisa kuujua wakati na mda uliopo na utakaokuja kwamba watu wazijue Siri za rohoni za MUNGU na pia Siri zao zifumbuliwe na watu wajirekebishe.   ​*Ko tunapozungumzia makanisa saba tunamaanisha mapungufu yaliyopo ndani yetu ambayo yanaweza kutufanya tusifike mbinguni au kusababisha tusione utofauti na upya kwenye maisha yetu ya kimwili na kiroho.    ​Kanisa la efeso. (kanisa la kwanza) Ufunuo 2:2a   ​Lilikuwa ni kanisa zuri sana. Lilikuwa na linaj...

Ukiokoka unakuwa mtu wa namna gani?

​ 09 Feb 2025 ​ Ukiokoka unakuwa ni mtu wa namna Gani? Amani Ernest Kyamba. ​Hili somo linaenda kujibu maswali mengi kama yafuatayo: ~wengine hawajaokoka mbona wanafanikiwa? #wengine wapo kanisani wanasali hawaishi kiroho lakini wanafanikiwa kwenye kazi zao ~wengine wanatoa zaka na sadaka ila hawafanikiwi. ​hayo maswali ni sample tu ya viwakilishi vingi vya maisha ya wokovu ambayo YESU Kristo anataka tuishi. lakini zaidi Mimi nagusia mahusiano yetu ya kiroho na YESU Kristo ambaye ndiye ukamilifu wa Sheria (pendo ndilo linaikamilisha Sheria) ​#mithali 3:5 kuokoka ni kuvua mwili, Roho na akili chini (za zamani) na kupokea vipya. Ni kumwabudu MUNGU pamoja na wale wenye uhai nanne na wazee ishirini na wanne jinsi wanavyodondosha taji zao na utukufu wao mbele za MUNGU ufunuo 4:10-11 kwamba wenyewe wanabaki hawana taji Wala utukufu wowote ule . basi na wokovu halisi ni kwamba unavua vyote vya kibinadamu (akili, plani za kibinadamu na vyote) unakuwa huna kitu unabaki mkiwa Tena...

Usijiamini

​ 04/02/2026 ​ Usijiamini mwanadamu. (Ufarisayo na jinsi ya kuushinda) ​#Samsoni alijiamini akaamka kama ilivyo kuwa ada kumbe hayupo kwenye mfumo. #farisayo alijiamini sana mbele za MUNGU kuliko mtoza ushuru na mtoza ushuru ndo aliyehesabiwa haki zaidi kuliko farisayo. #wale watu walikuwa wanasema BWANA, BWANA hatukufanya unabii kwa jina lako,na kwa jina lako kutoa Pepo na huduma. kilicho wafanya wapotee ni kujiamini kwao kutokana na ishara yaani kuziamini ishara kuliko MUNGU. na sisi tunajiamini sana kutokana na tunavyoonekana kwa watu (ishara za utakatifu) tunasahau kuwa je tunaonekanaje kwa MUNGU wa mbinguni?. #kilichomfanya shetani awe mwasi kule mbinguni ni kwa Sababu alijiamini sana kwamba yeye na wazo lake ni Bora sana. #kilichomfanya nabii yule afe pale ni kwa kuwa hakujiamini kuwa neno la lililomwambia kuwa asile af yeye akala kwa neno la yule nabii mzee. i falme 13:1-30. #je ni kwamba MUNGU alitaka yule nabii kijana afe? Hapana, ila alothibitisha jinsi watu tunavyoam...

Kwa nini umeokoka?

04/02/2026 ​ Kwa nn umeokoka?/mtazamo wako ndio unaokuvuta!! Fellow SOGH Amani Ernest Kyamba ​Je ni kwa Sababu unaikimbia dhambi au ni kwa Sababu unataka umwone MUNGU..ukimwona MUNGU Moja kwa Moja utakuwa umeikimbia dhambi. watu wengi wanaokoka ili kuikimbia dhambi jambo ambalo linamweka MUNGU nafasi ya pili kwenye maisha Yao kwa kuwa wanataka kuikimbia dhambi ili kwa hivyo wamwone MUNGU. akati wokovu dhamira yake kuu ni kumwona MUNGU. kwa kuwa kumwona MUNGU na kumtafuta ndiko kuishinda na kuwa mtakatifu. ukisema kuokoka ni kuikimbia dhambi ambayo ni asili Yako kwa kweli hauwezi wewe peke Yako kwa kuwa ni asili ya mwili kurudi mavumbini, yaani kutenda dhambi kwa kuwa ukiweka dhamira kwa mtazamo wa chini basi lazima huo mtazamo ukurudishe chini. ​YESU alisema aliye wa juu huwaza yaliyo ya juu na hufikiri yaliyo ya juu tu wakolosai 3:2. Usiwe motivated na ulikotoka Bali kuwa motivated na ulipo na unaokwenda kwenye maisha ya kiroho na mwilini pia, maana MUNGU peke yake ni WA tangu ...